Mwanafunzi wa darasa la 6 akutwa amefungiwa ndani na mwanaume akimlazimisha kumuoa, Mwanafunzi huyo asimulia ilivyokuwa – Video
Mwanafunzi wa darasa la 6 akutwa amefungiwa ndani na mwanaume akimlazimisha kumuoa, Mwanafunzi huyo asimulia ilivyokuwa - Video
Uongozi wa mtaa Geita mjini kwa kushirikiana na wakazi wa eneo hilo wamemkamata mwanaume aliyekuwa anaishi na mwanafunzi wa darasa la sita kwa kumlazimisha kumuoa.
Akizungumza jinsi tukio hilo lilivyotokea wifi wa mwanafunzi huyo, Bi Magret sabuholo amesema kuwa yeye alimuacha nyumbani nakuelekea sokoni mida ya asubuhi lakini baada ya kurudi akitoka sokoni hakumkuta na alimuulizia hadi ilipofika usiku hakuonekana ndipo hofu Ilitawala hali iliyowapelekea kutoa taarifa kwa uongozi wa mtaa huo .
Kwa upande wa kaka wa mwanafunzi huyo Bw Siajari Samsoni amesema kuwa mdogo wake alikuja kwa lengo la kumsalimia kutoka katika kjijij cha Samva kata ya Nyakabango wilaya ya Mleba mkoani Kagera kwani alikuwa amefunga shule.lakini amesikitishwa sana na tukio hilo ambalo limetokea katika familia yake.
Mbali na hilo Mwenyekiti wa mtaa Geita mjini Bw salvatory Danielly amesema kuwa mara baada ya kupokea taarifa hizo alichukua jukumu la kuandika barua ili kuelekekea katika kituo cha polisi kwa ajili ya kupata msaada wa kwenda kuwakamata.
Bongo5 ilipata nafasi ya kuzungumza na binti huyo mara baada ya kutoka hospitalini ambapo ameeleza kuwa mwanaume huyo alimshawishi kuwa atamuoa endapo atamkubalia.
By Ally Juma.