Burudani
Mwandishi mahiri wa vitabu na daktari mstaafu Ben Carson atangaza kuwania urais wa Marekani
Mwandishi mahiri wa vitabu na daktari wa upasuaji mstaafu, Ben Carson ametangaza nia ya kuwania urais wa Marekani mwaka 2016.
Carson alitangaza nia hiyo kwenye umati jijini Detroit anakoishi.
Mkuu huyo wa zamani wa kitengo cha ‘pediatric neurosurgery’ kwenye hospitali ya Johns Hopkins hajawahi kugombea nafasi yoyote ya uongozi.
Lakini ni mtu maarufu kwa hoja zake na atajaribu kuhamishia mafanikio yake kama mwandishi na mzungumzaji kwenye kampeni za urais zenye ushindani mkali.
“I’m Ben Carson and I’m a candidate for president,” aliuambia umati wa watu.
Ataingia kuwania urais kupitia chama cha Republican.