Michezo

Nahitaji pongezi kuifunga Tottenham – Mourinho

Meneja wa klabu ya Manchester United, Jose Mourinho amesema kikosi chake cha mashetani wekundu (The Red Devils) kinastahili kupongezwa kwa kuifunga Tottenham ambayo imefanya vizuri katika michuano ya klabu bingwa barani Ulaya.

Meneja wa klabu ya Manchester United, Jose Mourinho

Mourinho ambae nimiongoni mwa makocha wachache wenyemaneno mengi katika ligi ya Uingereza ameyasema hayo hii leo katika mkutano wake na waandishi wa habari.

“Tottenham imeifunga Liverpool mabao 4-1 ikaifunga Real Madrid 3-1,lakini wameshindwa kufanya hivyo dhidi yetu bila shaka wachezaji wamgu wanastahili pongezi,”amesema Mourinho.

Timu ya Tottenham hapo jana usiku imefanikiwa kuchomoza na ushindi wa jumla ya mabao 3-1 mbele ya mabingwa watetezi klabu ya Real Madrid katika dimba la Wembley huku Dele Alli akitupia mawili na Christian Eriksen akimalizia karamu hiyo ya mabao.

Spurs imechomoza na ushindi huo wa kihistoria ndani ya klabu hiyo ikiwa ni sikuchache tu toka ikubali kipigo cha bao 1-0 kutoka kwa Manchester United lilofungwa na Anthony Martial mchezo wa ligi kuu nchini Uingereza.

Mourinho amesisitiza United inastahili pongezi kwa kuishushia kipigo Tottenham ambayo imechomoza na ushindi wa mabao 4-1 dhidi ya Liverpool mwezi uliyopita.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents