Shindano la kwanza la karaoke barani Afrika, Tecno Own The Stage lilimalizika Jumapili ya Feb 7 na ushindi kwenda Nigeria kwa Shapeera.
Mshindi huyo aliondoka na kitita cha $25,000 pamoja na mashavu mengine.
Hata hivyo mshindi wa pili, Nandy wa Tanzania naye aliondoka na mtaji wa kutosha kuanzisha safari yake muziki. Alijishindia $15,000 ambazo ni takriban shilingi milioni 36.
Pia alipata shavu la kunolewa kimuziki chini ya label ya Nigeria, Chocolate City ambayo ni nyumbani kwa wasanii wakuwa kama M.I., Ice Prince, Victoria Kimani na wengine.
Tulipiga story na Nandy kwenye video hapo juu.