Burudani
Nje ya muziki mimi ni mfanyabiashara – Dogo Janja
Dogo Janja anafanya muziki, lakini kutokana na biashara ya muziki kuwa haina uhakika wa lini msanii ataingiza kiasi gani kama ilivyo kwa wafanyakazi wenye uhakika wa mshahara kila mwisho wa mwezi, anacho kitu kingine ambacho anakifanya kumuongezea kipato.
Janjaro ambaye anafanya kazi chini ya Madee na Tip Top Connection, amesema kuwa anafanya biashara ndogo ndogo ambazo zinampa uhakika wa kuingiza angalau shilingi elfu 10 kwa siku.
“Kitu nachoweza kusema mishe nje ya muziki ni mfanya biashara tu, nina nyenzo kadhaa zinazoweza kuniingizia elfu 10 elfu kwa siku” alisema Janjaro kupitia E-Newz ya East Africa TV.