Burudani
Pete ya Rihanna kwenye red carpet yazua maswali mengi kwa mashabiki
Tetesi za ukaribu wa Drake na Rihanna zimezidi kukua baada ya Rihanna kuonekana akiwa amevaa pete ya almasi yenye thamani ya $1m.
Jumapili usiku kulifanyika tamasha la ugawaji tuzo maarufu kama Billboard Music Awards lililoudhuriwa na mastaa kibao ambapo Rihanna alikuwa ni mmoja ya wageni waliohudhuria na kutumbuiza lakini aliwashangaza mashabiki wake kwenye red carpet baada ya kuonekana akiwa amevaa pete kwenye kidole chake cha nne kwenye mkono wa kushoto ambayo ni ishara kuwa ni pete ya uchumba.
Hivi karibuni Rihanna alimshirikisha Drake kwenye wimbo wa ‘Work’ huku pia tetesi za wawili hao kuwa wapenzi tena zikienea na kuvuta picha kuwa tayari Drake ndiyo aliyemvalisha pete hiyo ya thamani.