Burudani
Pharrell Williams ajiunga na shindano la ‘The Voice US’
2013 na 2014 ni miaka ya ‘furaha’ kwa Pharrell Williams. Hitmaker huyo wa The Neptunes amekula shavu la kusainishwa kama kocha wa shindano la ‘The Voice’.
Muimbaji huyo mwenye miaka 40 atakijaza kimoja ya viti vyekundu vya shindano hilo la kuimba katika msimu wa saba. Williams anayeendelea kuhit na wimbo wake ‘Happy’ anaziba nafasi ya CeeLo Green, aliyeondoka baada ya kuwepo kwa misimu minne.
Makocha wengine watatu wa shindano bado hawajatangazwa.