Picha: Mashindano ya Miss Tanzania 2016 yazinduliwa
Mashindano ya Miss Tanzania yaliyowahi kufungiwa kwa miaka miwili kufuatia skendo ya Sitti Mtemvu yamezinduliwa tena.
Mkurugenzi wa kampuni ya Lino International Agency, Hashin Lundenga akiongea kwenye uzinduzi huo
Hafla ya uzinduzi wa msimu mpya wa mashindano hayo ilifanyika kwenye hoteli ya Ramada Resort iliyopo Kunduchi, Dar es Salaam.
Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye (kushoto) akifurahi jambo na mmoja wa wajumbe wa kamati ya Miss Tanzania. Wengine ni Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa la Taifa, Geogrey Mngereza na Lundenga
Mgeni rasmi alikuwa Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye. Wengine waliohudhuria ni pamoja na Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa la Taifa, Geogrey Mngereza, warembo waliowahi kushika taji la Miss Tanzania miaka iliyopita na mawakala wanaoandaa mashindano ya Miss Tanzania katika ngazi mbalimbali hapa nchini.
Kutoka kushoto ni Miss Tanzania 1998, Basila Mwanukuzi, Miss Tanzania 1999, Hoyce Temu, Miss Tanzania 2008, Nasreen Kareem pamoja na Miss Tanzania 2014/2015, Lilian Kamazima wakipozi katika picha ya pamoja kwenye uzinduzi wa Msimu mpya wa mashindano ya urembo ya Miss Tanzania 2016
Linah akitumbuiza kwenye hafla hiyo
Miss Tanzania 2014/2015, Lilian Kamazima na Miss Tanzania 1999, Hoyce Temu
Picha: Mo Dewji Blog