Michezo
Kauli kuhusu ushoga yamfanya Pacquiao apigwe marufuku kuingia kwenye mall maarufu ya LA
Baada ya kampuni ya Nike kusitisha mkataba na bondia wa Ufilipino, Manny Pacquiao kufuatia kauli yake kuwa mashoga ni wabaya zaidi ya wanyama, mall maarufu ya jijini Los Angeles, Grove imempiga marukufu.
Mmiliki wa mall hiyo, Rick Caruso amedai kuwa uamuzi huo umechukuliwa kwakuwa watu wengi wanaojihusisha na mapenzi ya jinsia moja ni wateja wa mara kwa mara wa mall hiyo na kwamba wana haki ya kujisikia vibaya.
“Hivyo Manny Pacquiao hakaribishwi tena,” alisema.
Kauli hiyo iliyowakasilisha watu wengi wanaojihusisha na mapenzi hayo ilimfanya aombe radhi.