Burudani
Producer C9 asaini mkataba wa usimamizi na Panamusiq
Producer wa muziki Charles Francis aka C9 ameasini mkataba wa muda mrefu wa usimamizi na kampuni ya Panamusiq Ltd.
Panamusiq wameandika kwenye taarifa kwa vyombo vya habari:
“Panamusiq is pleased to announce the signing of Tanzanian top producer C9 who has entered a long term management contract with the Dar based music company.”
Producer huyo ameungana na wasanii ambao tayari walikuwa wameingia kwenye usimamizi wa kampuni hiyo akiwemo Feza Kessy na Linah.
Ben Pol naye aliwahi kusaini na kampuni hiyo lakini alivunja mkataba nao miezi mitano baadae baada ya pande zote mbili kukubaliana.