BurudaniVideos

Q-Chief aeleza namna alivyoweza kuachana na madawa ya kulevya (Audio)

“Kuingia kwenye madawa ya kulevya ni rahisi sana, la kutoka ni ngumu,” ni maneno ya Q-Chief katika mahojiano na kipindi cha Amka na Choice FM.

Kwa mujibu wake mwenyewe, Chief ni miongoni mwa watu walioweza kujinasua kutoka kwenye matumizi ya madawa hayo yanayozidi kuwaangamiza vijana wa Tanzania.

Yeye aliwezaje kujinasua?

“Mimi I took my mind on a trip before making decision,” anasema msanii huyo.

“Ni kwamba nilikuwa nikiwatazama watoto wangu machoni naona maumivu, I saw tears wengine hawakuweza kuhandle ile situation nikajikuta nalia nao, tunalia pamoja. Lakini ikanifikia kipindi sasa nawakimbia kwa maana wakiniona wanazidi kulia, nikajiuliza nitaendelea kuwaumiza hawa malaika mpaka lini? Na niliwaleta duniani na wao wawe na faraja na kesho my father was one two, three.. ” anasema.

“Lucky me nilikaa nao chini na kuanza kuonesha mabadiliko mwenyewe. Changes starts with you. Kwasababu wewe unapobadilika, mtu wa jirani ataona mabadiliko yako. Lakini ukichukua muda mrefu kumuonesha jirani mabadiliko yako of course hatoamini sababu ukizungumzia unga naamini it’s very hard mtu kutoka,” amesisitiza Chief.

“Ndio maana wasanii wenzangu wanatoka, wanarudi.”

Anadai kuwa amepokea simu zaidi ya 100 wakiwemo BBC akiulizwa aliwezaje kujitoa kwenye matumizi hayo, na akadai kuwa aliamua mwenyewe kwa kuelewa umuhimu wake na wala hakwenda sober wala kufanyiwa counseling yoyote.

Q-Chief amesisitiza kuwa si rahisi kabisa kwa wasanii walioathirika na madawa ya kulevya kuyaacha kwa kushinikizwa na watu, bali ni wao wenyewe.

Msikilize hapo juu alivyozungumza kwa hisia na kutoa ushauri muhimu.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents