Rais Magufuli awakaribisha Wakenya kuja kufanya biashara Tanzania
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli ameomba Wakenya kuja kufanya biashara Tanzania.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akisalimiana na mwenyeji wake Rais wa Kenya,Uhuru Kenyatta
Ameyasema hayo akiwa katika ziara ya siku mbili nchini humo na kuwaeleza kuwa wanaweza kuja kufanya biashara hata leo.
“Ninawakaribisha tena Wakenya wote wanaotaka kufanya biashara Tanzania, waje hata leo” amesema Magufuli. Dkt Magufuli yupo jijini Nairobi, katika ziara yake ya kiserikali ya siku mbili nchini humo.
Chini ni picha za mapokezi yake nchini humo.
Rais Magufuli akifurahia jambo na mwenyeji wake rais wa Kenya Uhuru Kenyatta akiwasili Ikulu Jumatatu hii
Rais Dkt Magufuli akisalimiana na naibu rais wa Kenya Mh. Willam Ruto
BY: EMMY MWAIPOPO