Habari
Rais Samia awatakia heri darasa la saba
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan kupitia ukurasa wake wa Twitter amewatakia heri wanafunzi wote wanaoanza mitihani yao ya kuhitimu elimu ya msingi hii leo Oktoba 5, 2022.
”Nawatakia kila la kheri wanangu wote mnaoanza mtihani wa darasa la saba leo. Mwenyezi Mungu awape utulivu na siha njema ili mfanye vizuri mitihani yenu. Serikali itahakikisha maandalizi ya miundombinu ya kuwapokea wote watakaoendelea na kidato cha kwanza mwakani 2023 inakamilika.”- Rais Samia Suluhu Hassan