Burudani

Rama Dee adai wasanii hawana haja ya kwenda kushoot video nje ya Tanzania

Msanii wa muziki wa R&B wa Tanzania, Rama Dee anashangaa jinsi wasanii wa muziki wa Tanzania wanavyokwenda nje kushoot video za muziki wakati ndani wana kila kitu.
Rama Dee 2

Muimbaji huyo ambaye aliachia wimbo ‘Kipenda Roho’ ambao unafanya vizuri, ameiambia BBC kuwa haoni kama ni sahihi wasanii wa ndani kwenda kufanya video zao za muziki Afrika Kusini.

“Hapa hapa kwetu kuna watu wanaweza kutengeza video nzuri bila shaka,” alisema Rama Dee. “Mimi huwa siamini issue ya Afrika Kusini au wapi, mimi naamini ukiwa na idea nzuri, kamera nzuri na unaweza kushare idea na director, munaweza kufanya kitu kizuri sana,”

Rama Dee yupu nchini Tanzania kimapumziko, kwa sasa anaishi na kufanya shughuli zake nchini Australia.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents