Habari
RC Makala atangaza hatari eneo la Kunduchi
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Amos Makala amelitangaza eneo la Kunduchi lenye Volcano ya Tope kuwa eneo la hatari na halifai kwa makazi na kuwataka Wananchi wa familia Tisa ambazo makazi yao yameathiriwa kuanza kuchukuwa tahadhari.
RC Makala amesema hayo alipotembelea na kukagua eneo hilo kujionea athari za Volcano hiyo na kulielekeza Jeshi la Polisi kuweka uangalizi Katika eneo hilo.
Aidha Mh. Makala amesema taarifa ya kitaalamu iliyowasilishwa ofisini kwake inaeleza kuwa eneo hilo halifai kwa makazi ndio maana amefika kuwataka kuchukuwa tahadhari wakati Serikali inaangalia hatua za kuchukuwa.
Pamoja na hayo ameelekeza eneo hilo kuwekewa alama za tahadhari ili kuwaepusha wananchi na maafa.