Michezo
Roy Hodgson atemwa na Liverpool
Kwa wadau wa soka na hasa mashabiki wa Liverpool, sio siri kwamba timu hiyo imeshuka daraja hadi nafasi ya 12 na vile vile kasi ya uchezaji kupungua kwa kiasi kikubwa ndani ya miezi michache.
Yote haya yamepelekea kutoswa kwa kocha mkuu wa Liverpool Roy Hodgson toka anfiled, baada ya kushauriana na wamliki wa klab hiyo na kufikia uwiano kutoendelea na mkataba wake. Mchezaji wa zamani, Kenny Dalglish ndiye atakayeshikilia nafasi ya umeneja kwa muda huu.
Hodgson aliyejiunga na klabu hiyo mnamo Julai 2010 amefanikiwa kuipeleka timu hiyo kushinda mechi 20 ndani katika ligi ya premier.
Kocha huyo amegoma kutoa tamko lolote kufuata kuondoka kwake.