Habari
Naibu Meya wa Arusha ajiuzulu
Siku chache baada ya mchafuko kati ya wanachama na viongozi wa CHADEMA na jeshi la polisi, naibu meya wa Arusha amejiuzulu kwa kile kinachosemekana ni ubatili wa matokeo ya kura yaliyofanyika mjini hapo Desemba 18, mwezi uliopita.
Micheal Kivuyo aliyepewa nadhifa hiyo kupitia chama cha cha TLP, Tanzania Labour Party ameeleza sababu ya kujiuzulu ni kufuatia kuungana na wananchi wenzake wakazi wa Arusha, kupinga kitendo cha polisi kuwapiga raia na kusababisha mchafuko wa amani ambapo hatimaye watu sita walipoteza maisha yao.
Kivuyo ameitaka serikali kurudia uchaguzi huo ambao unasemekana kuwa wenye utata.