Burudani

Said Fela azungumzia jinsi alivyowatengeneza vijana wa Yamoto Band kuwa na muziki tofauti

Said Fela ndiye aliye nyuma ya kuanzishwa kwa kundi la vijana wanne waitwao ‘Mkubwa na Wanawe’ au Yamoto Band ambao kwa sasa wametokea kupendwa. Hadi sasa vijana hao wana nyimbo mbili, Yamoto na Nitajuta iliyotoka wiki iliyopita.

Akiongea na Bongo5 Fela amesema aliitengeneza bendi hiyo kuwa na muziki tofauti. “Mimi niliangalia kwamba kuna watu wanaimba, akina Diamond wanaimba, akina Ali Kiba wanaimba,” amesema.

“Sasa nikasema nikiwatoa kwa mitindo ya akina Ali Kiba, akina Diamond, watoto watakosoa tobo la kutoboa. Kwahiyo nakasema ngoja nianzishe kitu, kwa kuanzisha kitu ndio nikaona wachukue muziki wa Kitanzania kidogo na hii kisasa kidogo halafu tupenye pale. Ndo maana unaona Yamoto wamekuja na muziki wao.”

http://youtu.be/ISakU2mTz7Y

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents