Burudani
SholoMwamba – Kwenda Kimataifa ni rahisi sana nikiwa Masta AY
Msanii wa muziki wa Singeli @officialsholomwamba amefunguka kwamba anaimani project yake mpya na @aytanzania itafika mbali zaidi na kuutangaza muziki wa singeli Kimataifa.
“Singeli Twista ni project iliyoandaliwa kwa hatua zote, na tuona kabisa njia ni nyeupe ya kwenda kimatafa, namuona Masta @aytanzania ambaye alifungua milango ya kwenda Kimataifa na ameshiriki katika project hii mwanzo mwisho,” alisema SholoMwamba.
Msanii huyo amewaomba mashabiki wake kukaa mkao wa kula kwaajili ya kazi hiyo pamoja na mambo mengine mazuri yanayokuja.