Burudani
Sisqo na kundi lake la Dru Hill kutumbuiza Kenya Jumamosi hii
Mark Althavean Andrews, maarufu kama Sisqó ni mwimbaji wa RnB kutoka Marekani ambaye alivuma mwishoni mwa miaka ya 90 na hits zake kama ‘Unleash the Dragon’, ‘Thong Song’ na zingine.
Sisqó pia ni lead singer wa kundi la ,ru Hill ambalo limewahi kutamba na nyimbo kama ‘How Deep Is Your Love’, ‘In My Bed’ na zingine.
Mwimbaji huyo na kundi lake la Dru Hill linaloundwa na yeye, Taio, Nokio na Jazz wamewasili Kenya tayari kuwapa burudani mashabiki wa nchi hiyo kwenye onesho litakalofanyika Jumamosi ya Oct 24.