Sitofanya Uasi baada ya mke wangu kufariki – Mrema
Mwenyekiti wa Chama cha TLP Augustino Mrema, amesema hatafanya uasi wa aina yoyote baada ya mkewe Rose Mrema kuaga dunia.
Mrema ameeleza hayo leo Oktoba 04, akiwa nyumbani kwake Mkoani Kilimanjaro ikiwa ni siku chache kupita tangu kufariki kwa mke wake.
“Nikisema ‘na-mmiss na-mmiss’ kweli, nimekubaliana na mke wangu sitafanya uasi wowote baada ya yeye kufariki. Nitafata nyayo zake. Kabla ya kufariki alituita kwa pamoja na watoto na wajukuu na kutuweka sawa. Watoto walikuwa wanakwaruzana lakini tumesikia na tutayaenzi yote ya mama,” Mrema.
Aidha Mrema amesema kabla ya Mkewe kufariki amemfanyia mambo makubwa ikiwa ni pamoja na kumuunganisha na Serikali na ndio sababu hata alipofariki aliweza kupokea salamu za rambi rambi kutoka kwa Rais na Waziri Mkuu
Bi. Rose Mrema, alifariki dunia Septemba 16, 2021 wakati akipatiwa matibabu katika hospitali ya Taifa Muhimbili kufuatia kupatwa na tatizo la shinikizo la damu, ambapo taarifa ya madaktari ilisema mishipa mitatu ilikuwa imeziba kwa muda mrefu.
BY : Fatuma Muna