Trip ya Jay-Z na Beyonce nchini Cuba yazua zogo
Wabunge wawili wa jimbo la Florida nchini Marekani, wanataka kufahamu iwapo serikali ya Marekani iliruhusu safari ya Jay-Z na Beyoncé nchini Cuba.
Wapenzi hao walikuwa nchini humo kusherehekea miaka mitano ya ndoa yao. Wawakilishi hao Ileana Ros-Lehtinen na Mario Diaz-Balart wamewasiliana na ofisi ya Foreign Assets Control at the Treasury Department kuuliza kama wapenzi hao walipata kibali halisi cha kuingia kwenye nchi hiyo ya kikomunisti.
Wakikasilishwa na picha za mastaa hao zinazowaonesha wakifurahia safari yao kwenye kisiwa hicho, wabunge hao wamewakosoa kwa kuiunga mkono serikali ya kidhalimu ya Raúl Castro kwa kumwaga mamalioni ya dola kwa kukaa kwenye hoteli za kifahari wakiwa na familia, marafiki na walinzi wao.
Wawili hao wameikosoa serikali ya Cuba na kutaka wapewe maelezo kuhusu aina gani ya kibali Mr and Mrs Carter walipata kuingia nchini humo.