Habari

Ulimwengu usiwe na wasi wasi na deni la Marekani- Biden

Rais Joe Biden wa Marekani amejaribu kuwahakikishia viongozi wa ulimwengu kuwa Washington haitoshindwa kulipa deni lake licha ya kiwingu kinachogubika mazungumzo ya kuongeza ukomo wa serikali yake kukopa.

Akizungumza kabla ya kukutana na viongozi wa kundi la mataifa manne linalofahamika kama QUAD pembezoni mwa mkutano wa G7 huko Hiroshima nchini Japan, Biden amesema hakuna sababu ya ulimwengu kuwa na wasiwasi juu ya deni la Marekani.

Amesema anaamini mazungumzo yanayoendelea kati yake na wabunge wa Republican yatazaa matunda, akipigia mfano kuwa duru ya pili na ya tatu ya mazungumzo hayo yamepata mafanikio fulani ya kutia moyo.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents