Habari
Video: Lord Eyez akiongelea kuhusu Weusi, maproducer anaopenda kufanya nao kazi na rappers anaowakubali
Wiki hii kwenye kipindi cha Trending Africa cha Times FM 100.5, Lord Eyez alifunguka mengi kuhusu asili yake, maproducer anaopenda kufanya nao kazi, tofauti ya Weusi na Nako 2 Nako, jinsi walivyosota na Joh Makini baada ya kuja Dar kurekodi na rappers wa Tanzania anaowakubali. Trending Africa huendeshwa na Raheem Da Prince, Moko Biashara na Dj R Guy. Itazame video ya interview hiyo.