Burudani

Video ya Mazoea imekula pesa nyingi sana – Billnass

Msanii wa muziki wa hip hop Billnass amedai uwekezaji mkubwa alioufanya kwenye video ya wimbo wake mpya ‘Mazoea’ ndio kitu ambacho kimeufanya wimbo huo kupokelewa kwa kasi zaidi.

Rapper huyo ameiambia Bongo5 kuwa video ya wimbo huo ni moja kati ya video zake alizowekeza pesa nyingi zaidi.

“Mamshukuru mungu ‘Mazoea’ inaenda vizuri na tayari kuna simu za show ambazo nimeanza kupigiwa ili kurudisha kile tulichokiwekeza kwa sababu Mazoea ni moja kati ya video zangu ambayo imekula pesa nyingi sana,” alisema Billnass.

Bill amewashukuru mastaa mbalimbali pamoja na mashabiki wake ambao wameonyesha kuusupport wimbo huo aliomshirikisha rapper mkongwe, Mwana FA.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents