Siku ya leo April 4, 2022 Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar Es Salaam likiongozwa na Kamanda Jumanne Muliro limewakamata vijana waliokuwa wakijaribu kuhujumu miundombinu ya Daraja la Tanzanite Dar es Salaam kwa kuiba baadhi ya vyuma katika daraja hilo.
Akizungumza na Vyombo vya Habari Kamanda anasema kuwa wahutumiwa hao wamekamatwa baada ya kukutwa wakijaribu kufungua baadhi ya vyuma na kutaka kuchukua kwaajili ya shughuli zao binafsi.