Leo ndio ile siku ya Kongamano kubw ala maji linalijulikana kama KONGAMANO LA KISAYANSI LA MAJI ambalo limezinduliwa na Naibu Waziri wa Maji Mhe. Eng. Maryprisca Mahundi katika ukumbi wa mikutano wa Mwl. Julius Kambarage Nyerere Posta jijini Dar Es Salaam.
Katika Kongamano hilo Taasisi za Serikali na binafsi zinakuwa na maonyesho ya Teknolojia, vifaa na bidhaa za kisasa zinazotumika katika kazi mbalimbali za kuwafikishia huduma ya majisafi, salama na ya kutosha wananchi.
Hadi sasa washiriki kutoka nchi za Kenya, Nigeria, Sierra Leonne, Afrika Kusini, Uganda na wenyeji Tanzania walidhithibitisha kuwasilisha matokeo ya tafiti zaidi ya 60.