Habari
Wabunge wapya CUF waapishwa
Mkutano wa Nane wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania umeanza leo ambapo katika kikao chake cha kwanza wabunge saba wa viti maalum walioteuliwa (CUF) wameapishwa.
Wabunge hao walioteuliwa hivi karibuni na Tume ya Taifa ya Uchaguzi(NEC) na wamekula kiapo cha uaminifu bungeni ili kuanza kulitumikia Bunge hilo na wananchi.
Wabunge waliopishwa ni Mhe. Alfredina Apolinary Kahigi, Mhe. Kiaza Hussein Mayeye, Mhe. Nuru Awadhi Bafadhili,Mhe. Rukia Ahmed Kassim, Mhe. Shamsia Aziz Mtamba, Mhe. Sonia Jumaa Magogo,Mhe. Zainab Mndolwa Amir.
Bunge linaendelea na sasa ni kipindi cha maswali na majibu.