Fahamu

Wafahamu viongozi wa Palestina na Israel waliotaka kuleta amani, mmoja akauawa kwa kupigwa risasi na mwingine kupewa sumu (+ Video)

Iwapo kuna viongozi wa Israel na Palestina ambao wangetamani sana kuwepo Amani kati ya Waisrali na Wapalestina basi ni aliyekuwa waziri mkuu Yitzhak Rabin na aliyekuwa kiongozi wa PLO na harakati za Wapalestina Yasser Arafat.

Hata hivyo miaka mingi baada ya viongozi hao kuaga dunia ,mapigano na uhasama baina ya watu wao yanaendelea na kusababisha maafa ya watu wengi na wengine kujeruhiwa .Je,walipigania nini viongozi hao na ni vipi walilipia gharama ya kutaka pawepo amani?

Mnamo tarehe 13 Septemba 1993, Arafat na Waziri Mkuu wa Israeli, Yitzhak Rabin, walitokea uwanja mdogo wa bustani wa Ikulu ya White House baada ya mazungumzo ya siri yaliyowezeshwa na wanadiplomasia wa Norway.

Pande hizo mbili zilitia saini Azimio la Kanuni, makubaliano yanayowaruhusu Wapalestina kujitawala katika Ukanda wa Gaza na mji wa Ukingo wa Magharibi wa Yeriko na badala yake PLO kutambua serikali ya Kiyahudi.

Lakini maswala ya kimsingi kama makazi ya Wayahudi kwenye ardhi inayokaliwa, mustakabali wa Wapalestina ambao walifanywa wakimbizi mnamo 1948 na mustakabali wa Jerusalem yaliachwa bila uamuzi.

Ingawa Arafat alirudi kwa ushindi huko Gaza mwaka uliofuata, mchakato wa amani ulijaa shida.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents