Burudani
Waimbaji Sanaipei na Anto Neosoul wa Kenya ni kati ya watangazaji 36 waliofutwa kazi kwa kushtukizwa na Nation Fm!
Mwishoni mwa mwezi uliopita kituo cha radio cha Nation Fm cha Kenya, kiliwafukuza kazi jumla ya wafanyakazi 36 wakiwemo mastaa wawili wa muziki, kwa mujibu wa ripoti za mitandao ya Kenya.
Mumbaji wa kike Sanaipei Tande pamoja na muimbaji wa ‘Paid My Dues’, Anto Neosoul ni miongoni mwa watangazaji wa kituo hicho waliokumbwa na fagio hilo la kushtukiza.
Bado haijawekwa wazi sababu iliyofanya uongozi wa kituo hicho kufikia uamuzi huo, lakini Anto aliandika kwenye akaunti yake ya Facebook kuwa Nation FM imewafukuza kazi kutokana na ukosefu wa fedha.
Hizi ni Tweets za Anto Neosoul na Sanaipei baada ya kupata taarifa za vibarua vyao kuota nyasi August 31, 2015.
Wafahamu zaidi Sanaipei na Anto Neoseoul kupitia video za nyimbo zao