Habari
Wakazi wa Dar, Pwani na Tanga wapewa tahadhari
Mamlaka ya hali ya hewa nchini Tanzania (TMA) imetoa tahadhari kwa wananchi kuwepo kwa hali mbaya ya hewa katika maeneo yote ya pwani kuanzia leo usiku mpaka Februari 7 mwaka huu.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Februari 05, 2018 imeeleza kuwa usiku wa kuamkia kesho kutakuwa na vipindi vifupi vya upepo mkali unaozidi kilomita 40 kwa saa na mawimbi makubwa yanayozidi mita 2 ambavyo vinatarajiwa katika maeneo ya mikoa ya Tanga, Dar es Salaam, Pwani, Lindi na Mtwara pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba.
Soma zaidi taarifa hiyo iliyotolewa na TMA;