Habari

Watanzania 200 kuwasili leo wakitokea Sudan kufuatia mapigano yanayoendelea nchini humo

Jumla ya Watanzania 200 wanatarajiwa kuwasili leo asubuhi katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere wakitokea Sudan kufuatia mapigano yanayoendelea nchini humo baina ya kikosi cha Jeshi la Sudan (SAF) na Kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF).

f249be18-9f23-4fa4-a8ad-9c5fed08c58b.jpeg

Ndege yao imeondoka saa 12:30 asuhuhi ya leo, Idadi hiyo inahusisha wanafunzi 150, watumishi wa Ubalozi 28, diaspora 22.

Wamo pia raia wa nchi za Marekani, Uingereza, Kenya, Uganda, Sierra Leone, Malawi, Zambia na Msumbiji ambao Wote kwa pamoja walisafirishwa kwa mabasi kwa siku mbili kutoka Khartoum, Al Qadarif, Metema hadi Gondar zaidi ya kilometa 900.

Baadaye walisafirishwa kwa ndege ndogo toka Gondar hadi Bole walikochukuliwa na ndege ya ATCL hadi Dar es Salaam, Tanzania.

KUREJEA KWA WATANZANIA KUTOKA SUDAN

Watanzania 200 na baadhi ya Waafrika wa nchi nyingine waliokuwa Sudan wanatarajiwa kuwasili Dar es Salaam kati ya saa 10 hadi 11 Alfajiri ya tarehe 27 April 2023.

Safari ya kurejea nyumbani ilianzia Khartoum Kwa mabasi, majira ya saa 7.30 mchana ya tarehe 24 April 2023 na kuelekea Mji wa Al Qadarif ambao upo takriban kilometer 420 kutoka Khartoum.

Msafara ulifika Al Qadarif usiku na kulazimika kulala kutokana na usalama na kuondoka asubuhi ya tarehe 25 April 2023 kulekea Mji wa Metema, Ethiopia ambao unapakana na Sudan. Metema Iko kilemet 161 kutoka Al Qadarif.

Kutoka Metema, Msafara ulianza safari kuelekea Mji wa Gondar, Ethiopia ambao uko kilometer 220.

Kutoka Gondar Watanzania hao 200 na raia 10 wa nchi nyingine za Afrika walisafiri Kwa ndege kwenda uwanja wa Bole, Addis Ababa.

Kutoka Addis Ababa wata chukuliwa na Ndege ya Tanzania (ATCL) dreamliner kuja Dar es Salaam.

Summary ya route:
1. Kutembea Kwa miguu kutoka kwenye Makazi yao kwenda meeting point – International University of Africa (IUA), Khartoum huku mapigano yakiendelea (hatari tupu).

2. Safari kutoka IUA-Khartoum kwenda Al Qadarif (420km) Kwa mabasi na kulala usiku mmoja

3. Kubadilisha mabasi na kusafiri kutoka Al Qadarif hadi Metema mpakani Ethiopia (160km).

4. Kusafiri Kwa mabasi tena kutoka Metema kwenda Gondar Airport, Ethiopia (220km).

5. Kusafiri Kwa ndege kutoka Gondar kwenda Bole – Addis Ababa.

6. Kusafiri Kwa ndege ATCL kutoka Bole Addis Ababa hadi Dar es Salaam.

Abiria wengi wa nchi nyingine watakabidhiwa Kwa Balozi zao Addis Ababa. Raia mmoja wa Uingereza mwenye asili ya Tanzania atasafiri hadi Dar es Salaam.

NB: Uwanja wa ndege wa Gondar ni mdogo hivyo imebidi zitumike ndege 2 kuwasafirisha kutoka Gondar hadi Bole, Addis Ababa

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents