Burudani

Yemi Alade, Chameleone na Tekno kuungana na mastaa wa Bongo kwenye Fiesta ya Dar

Yemi Alade alishinda tuzo ya msanii bora wa kike, na Tekno akachukua ya msanii bora aliyechipukia kwenye tuzo za MTV MAMA 2016 – hawa wawili hawakwepeki na hakuna ubishi ni miongoni mwa wasanii wa moto zaidi Afrika kwa sasa.

fiesta

Wapopo hao wametajwa kutumbuiza kwenye kilele cha tamasha la Fiesta, litakalofanyika jijini Dar kwenye viwanja vya Leaders, November 5.

Hiyo sio mara ya kwanza wawili hao kuja Dar. Supastaa na nguli wa muziki wa Uganda, Jose Chameleone naye atatumbuiza kwenye show hiyo.

Wasanii wengine watakaopanda jukwaani siku hiyo ni pamoja na Alikiba, Raymond, Mr Blue, Belle 9 ba wengine. Bado haijajulikana ni msanii yupi kutoka Marekani atakayetumbuiza mwaka huu.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents