Burudani
Young Thug kuungana na Diamond, Tamar Braxton, Maxwell na wengine kwenye tamasha la ‘BET Experience Africa’
BET wamemwongeza rapper Young Thug wa Marekani, kwenye orodha ndefu ya wasanii wa kimataifa na kutoka Afrika watakaotumbuiza kwenye tamasha la ‘BET Experience Africa’ lililopangwa kufanyika December 12, jijini Johannesburg, Afrika kusini.
Rapper huyo ataungana na wasanii wengine waliokuwa tayari wametangazwa kutumbuiza akiwemo Diamond Platnumz, Tamar Braxton, Maxwell, Flavour na Aka.
Diamond ndiye msanii pekee wa Afrika mashariki aliyetajwa kutumbuiza kwenye tamasha hilo hadi sasa. Wasanii wengine wataendelea kutajwa.
Hii itakuwa ni mara ya kwanza kwa tamasha hilo kufanyika Afrika.