Burudani
Apple yauza iPhone milioni 48 katika miezi mitatu
Kampuni ya Apple imeuza simu za iPhone milioni 48 katika kipindi cha miezi mitatu iliyopita – yaani ni sawa na Tanzania nzima imenunua simu hizo.
Mauzo hayo yamesababishwa pia na uzinduzi wa simu zake mpya 6S na 6S Plus mwezi uliopita. Mauzo hayo yameifanya kampuni hiyo kupata faida ya robo ya mwaka kuliko ilivyotarajiwa.
Kwa ujumla katika kipindi hiki Apple imeingiza takribani dola bilioni 234.