Michezo
Arsene Wenger adai Walcott ndiye tegemeo la Arsenal
Michuano ya vilabu bingwa Ulaya inaanza September 15 ambapo klabu ya Arsenal inaanza kwa kukabiliana na Dinamo Zagreb katika uwanja wa Stadio Maksimir siku ya Jumatano.
Kocha wa timu hiyo Arsene Wenger amekuwa akikosolewa kwa kushindwa kununua mshambuliaji mpya, lakini anasema kuwa anakiamini kikosi chake na kwamba Theo Walcott ndio jibu la safu yake ya mashambulizi.
Wenger amesema kuwa ni muhimu kwa kikosi chake kutoshindwa katika mechi ya kwanza ya michuano hiyo nchini Croatia.