Michezo
Arturo Vidal akamilisha uhamisho wa £28m kwenda Bayern Munich
Kiungo wa timu ya taifa ya Chile, Arturo Vidal amejiunga rasmi na klabu ya Bayern Munich ya Ujerumani kutoka Juventus ya Italia kwa uhamisho wa pauni milioni 28.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28 amesaini mkataba wa miaka minne baada ya kufuzu vipimo vya afya mjini Munich.
Mkataba huo wa miaka minne na FC Bayern utamuweka Munich hadi mwaka 2019.