Michezo
Ballack achimbwa Mkwara
Kocha wa timu ya taifa ya ujerumani,Joachim Loew amesema nahodha wake Michael Ballack anatakiwa kuwa fiti uwanjani ili kuitetea nafasi yake mara baada ya kutoka majeruhi.
Ballack 34 anatarajiwa kurejea uwanjani hivi karibuni baada ya kusumbuliwa na maumivu ya goti muda mrefu kwenye mguu wa kushoto,akiwa amecheza mechi tatu katika klabu yake ya Leverkusen tangu alipo tua msimu huu akitokea Chelesa ambapo ameichezea timu ya taifa ya Ujerumani mechi 79.
Kukosekana kwake kumesababisha kiungo huyo wa Real Madrid kucheza nafasi yake akishirikiana na Bastian Schweinsteiger wa Bayern Munich,
‘Bado anahitajika sana’, alisema Loew.