Michezo
Barcelona yafulia mbaya
Taarifa ya ukaguzi mpya wa mahesabu katika klabu ya Barcelona uliofanywa chini ya Rais wao mpya Sandro Rossell imefichua kwamba mabingwa hao wa La Liga,’Ligi kuu ya Hispania’ walipata hasara ya mapato baada ya kodi inayofikia Euro million 77.1
katika mwaka wa fedha wa 2009/10 na sio faida ya Euro 11 kama ilivyoripotiwa na bodi ilyopita ya wakurugenzi wa timu hiyo.
Hasara hiyo ambayo mabingwa hao wamedai kuwa ni ya kwanza kwao katika kipindi cha miaka saba imeonyesha ni kwa namna gani klabu nyingi za Hispania zilivyo na tatizo la kifedha.