[youtube]http://www.youtube.com/watch?v=7rPpJGktkKg[/youtube]
Mwanamuziki Bob Junior amesema amefurahia sana kwa kitendo cha kupewa mwaliko na shule ya msingi ya Walemavu Jeshi la Wokovu. Bob Junior ambaye alifika shuleni hapo kwaajili ya kuwaliwaza watoto hao kutokana na hali zao, hali hiyo ilipelekea watoto hao kumtunga jina kwa kumteua kuwa Rais wa shule hiyo ya Jeshi la Wokovu.
Wanafunzi hao pia waliombwa kununuliwa vifaa mbalimbali, ikiwemo gitaa na vingine kwakuwa hata wao pia wanania ya kuwa wanamuziki na wengine kuwa waandaaji wa muziki ‘Producer’.
Katika shule hiyo aambayo kuna walemavu tofauti tofauti, ilikuwa hajawahi kutembelewa hata na msanii mmoja, jambo linalopelekea kujiona wapweke. Bob Junior amesema kutokana na roho ya kiimani aliyokuwa nayo, atahakikisha anawatimizia kile ambacho wamekuwa wakikihitaji kulingana na uwezo wake utakapoishia.