Michezo
Breaking: Arsenal yatangaza kumtimua kazi Unai Emery na majukumu kukabidhiwa kocha huyu
Klabu ya Arsenal imetangaza rasmi hii leo kumtimua kazi kocha wake, Unai Emery kupitia mitandao yake ya kijamii.
Arsenal imesema kuwa vijana wao kuanzia sasa watakuwa chini ya Freddie Ljungberg baada ya kuachana na Unai Emery.
Ni muda mrefu Unai Emery amekuwa akihusishwa na kutimuliwa kazi ndani ya Arsenal hasa kutokana na mwenendo mbaya ambao unapitia timu hiyo.