Burudani

Diamond: Kuna msikiti ninaujenga Mtwara

Diamond amejitolea kujenga msikiti.

Hitmaker huyo wa ‘Marry You’ amesema kwa sasa anajenga msikiti huo lakini upo mkoani Mtwara.

“Mimi nakushukuru sana mama yangu, asante sana. Naamini kabisa nitakuja Mtwara, Mtwara kule sasa hivi kuna msikiti ninaujenga na inshallah nikimaliza nitaenda kuuzindua,” alisema Diamond Jumamosi iliyopita kwenye sherehe ya 40 ya mtoto wake Nillan iliyofanyika nyumbani kwake Madale.

Diamond alisema maneno hayo wakati akimshukuru mama mmoja ambaye alimkabidhi viwanja viwili vya hekta 17 kwa kila kimoja huku kimoja kikiwa ni kitalu cha gypsum.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents