Burudani

DMX atupwa jela mwaka mmoja

Rapper kutoka nchini Marekani anayeunda kundi la Ruff Ryders, DMX amehukumiwa kifungo cha mwaka mmoja jela kwa kosa la kukwepa kulipa kodi.

 DMX alikamatwa July mwaka jana, kwa mujibu wa CBS rapper huyo anadaiwa kiasi cha dola milioni 1.7 ambapo inasemekana alifungua akauti benki nyingine na kutumia jina jingine ili kukwepa kodi.

DXM alikuwa akikabiliwa na mashtaka 14 ya ukwepaji kodi, hata hivyo alilipa faini ya dola 5000,000 za Kimarekani kinyume na hapo angetumikia kifungo cha miaka 44 jela.

Imeripotiwa kuwa DMX ameingiza zaidi ya dola milioni 2.3 kwa mwaka 2010 hadi 2015 lakini msanii huyo alikwepa kulipa kodi. Rapper huyo ni baba wa watoto 15.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents