Michezo

Federer ampiga Mkorea na kutinga nusu fainali Indian Wells

Mchezaji tennis, Roger Federer amefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya michuano ya Indian Wells na kuendelea kulinda heshima yake ya kuwa namba moja kwa viwango vya ubora duniani.

Federer amefanikiwa kutinga hatua hiyo siku ya hapo jana siku ya Alhamisi usiku baada ya kumshinda Mkorea Kusini, Chung Hyeon kwa jumla ya seti 7-5 6-1.

Mchezaji huyo mwenye umri mkubwa zaidi katika tennis anatarajia kukutana na Borna Coric, ambaye amemfunga Kevin Anderson kwa seti 2-6 6-4 7-6.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents