Haina jinsi, Juan Cuadrado akabidhi jezi kwa mwenye namba yake
Baada ya kukamilika kwa uhamisho wa Cristiano Ronaldo kutua klabu ya Juventus, mashabiki wa Turin wanahitaji mchezaji huyo kukabidhiwa jezi ya namba yake halisi.
Katika zoezi hilo la jezi anaepoteza zaidi ni kiungo wa Colombia, Juan Cuadrado ambaye anavaa namba saba kabla ya ujio wa Ronaldo.
Cristiano Ronaldo mwenye umri wa miaka 33 amejiunga na Juventus ya nchini Italia juzi kwa dau la pauni milioni 105 akitokea Real Madrid.
Más bienaventurado es dar que recibir; bendiciones 🙏🏾 Panita @cristiano en esta nueva aventura 💪🏾💪🏾#FinoAllaFine #ForzaJuve🏳️🏴 pic.twitter.com/MYAMcjVyxi
— Juan Cuadrado (@Cuadrado) July 11, 2018
Ronaldo ambaye ni mshindi mara tano wa Ballon d’Or ametumia misimu tisa Madrid baada ya uhamisho wake wa pauni milioni 80 akitokea Manchester United huku akiondoka na kuwacha rekodi ndani ya klabu hiyo kwa kufunga jumla ya mabao 451.
Nahodha huyo wa Ureno ameondoka Real baada ya kushinda mataji mawili ya La Liga titles, mawili Copa del Rey na mataji manne ya klabu bingwa barani Ulaya.