Habari

Hakimu aamuru mtandao wa Whatsapp kufungwa nchini Brazil kwa masaa 72

Hakimu mmoja nchini Brazili amefunga mawasiliano ya mtandano wa simu kwa njia ya whatsapp kwa saa 72.

150708110507_whatsapp_logo_512x288_afp_nocredit

Hakimu huyo Marcel Montalvao amesema kampuni inayomiliki mtandao huo imeshindwa kusaidia kutoa taarifa katika kesi ya uhalifu.

Mwezi Machi, Montalvao aliamuru kukamatwa kwa afisa mwandamizi wa Facebook katika nchi za Kilatini bwana Diego Dzoran baada ya kukataa kutoa ushirikiano katika uchunguzi dhidi ya dawa za kulevya.

Wamiliki wa mtandao huo wa Whatsapp ambao pia wanamiliki mtandao wa Facebook wamesema kuwa wamekatishwa tamaa na kitendo hicho kwa kuwa wamekuwa wakitoa ushirikiano wa kutosha mahakamani.

Mtandao huo umekuwa ukifungiwa mara kadhaa nchini Brazil kwa miezi michache ya karibuni kwa sababu zinazofanana na hizo.

Source:BBC

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents