Michezo

Hali ya Rigobert Song yaendelea vizuri, ahamishiwa nchini Ufaransa

Hali ya mchezaji wa zamani wa timu ya taifa ya Cameroon na nahodha wa timu hiyo, Rigobert Song imedaiwa kuendelea vizuri baada ya kukimbizwa hospitali ya mjini Yaounde Jumapili hii baada ya kuugua ghafla na kuanguka wakati akiwa nyumbani kwake huko Odza. Alishambuliwa na kiharusi.

928422_650483625016814_241768128_n

Song alikuwa akitumia mashine za kupumulia tangu siku aliyofikishwa hospitalini hapo lakini kwa sasa kwa mujibu wa taarifa ya daktari Louis Joss Bitang imesema kuwa hali ya mchezaji huyo inaendelea vizuri kwakuwa hapumulii mashine kwa sasa na amepelekwa nchini Ufaransa kwa ajili ya kupata matibabu zaidi.

“He has come out of his coma and the oxygen has been disconnected. His high blood pressure has returned to normal and the cerebral haemorrhage has been controlled. A medical aircraft will be in Cameroon in (Tuesday) he morning, we will have a working session with the French team and then he will be flown to France,” amesema daktari Bitang.

Song amewahi kuichezea Cameroon jumla ya mechi 137 na kufunga magoli 5 na aliwahi kuchezea timu ya Liverpool na West Ham United lakini pia aliwahi kuifundisha timu ya taifa ya Chad mwaka 2015.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents