Hassan Isihaka kuikabili derby ya Sukari Mtibwa V Kagera
Beki kisiki wa wana tam tam aliyekuwa anasumbuliwa na majeraha yaliyomuweka nje kwa takribani miezi mitatu, Hassan Isihaka amesha anza mazoezi na wenzake na yupo tayari kwa derby Mtibwa Sugar dhidi ya Kagera Sugar , mtandao wa klabu www.mtibwasugar.co.tz umezungumza na daktari wa Mtibwa, Mussa Juma ili kutaka kujua hali za kiafya za wachezaji katika timu ilivyo kwa sasa.
“Hali ni shwari katika timu wote wako sawa kikubwa ni kurudi kwa Hassan Isihaka na tumemruhusu kufanya mazoezi ya kila aina na ni ruksa kutumika katika mchezo wowote,” amesema daktari Juma.
Mussa Juma ameongeza “Majeruhi waliobaki kwa sasa ni Haruna Chanongo, Shaban Kado na Salum Kanoni, na hawa watakosekana katika mchezo ujao dhidi ya Kagera ” Juma
Kikosi cha wana tam tam kinaendelea na mazoezi yake katika uwanja wake wa nyumbani chini ya mkufunzi wake mkuu Zuber Katwila “Puchetino” kikijiwinda kwa ajili ya mchezo dhidi ya Kagera Sugar.
Rekodi za Head to Head
Kuelekea mchezo huo wa Jumapili ya November, 9 rekodi baina ya timu hizi mbili zinapokutana uwanja wa Manungu , katika michezo saba iliyopita Mtibwa Sugar wamefanikiwa kushinda michezo 5 na kutoka sare 2 na hawajapoteza dhidi ya Kagera katika uwanja wao wa nyumbani.
Mchezo wa mwisho kuchezwa katika uwanja wa Manungu baina ya timu hizi mbili ilikuwa September 17,20016 Mtibwa Sugar ilifanikiwa kuwanyuka Kagera Sugar 2-0 , magoli ya Mtibwa Sugar yalifungwa na Ibrahim Rajab “Jeba” na Haruna Chanongo.