Michezo
Hiki ndicho alichofanya Jose Mourinho kwa wazee waathirika wa Virusi vya Corona
Kocha Mkuu wa Tottenham, Jose Mourinho ameamua kutumia kipindi hiki ambacho ligi nyingi zimesimama kujitolea kuwasaidia wazee walioathirika na mlipuko wa virusi vya corona.
Mourinho ameamua kutumia muda wake kwa kuwasaidia kuwapelekea chakula karibu na uwanja wa mazoezi wa Spurs katika eneo la Enfield.
”Nipo hapa kutoa msaada kwa wazee Enfield, unaweza kuchangia chochote, chakula, pesa au kujitolea.” Amsema Mourinho.
Sio Mourinho pekee aliyoonyesha mfano huo wa kuigwa bali hata mchezaji, Toby Alderweireld ameonekana akitowa misaada katika kipindi hiki kigumu ambacho dunia inapambana na janga la virusi vya corona.
https://twitter.com/LoveUrdoorstep/status/1242167748672851968?s=20