Michezo
Ibrahim Ajib wa Simba SC achukua tuzo ya mchezaji bora wa Mwezi
Klabu ya Simba ilianzisha tuzo ya mchezaji bora wa mwezi kuanzia mwezi September 2015. Jana Feb 28 baada ya mechi ya Kombe la maarufu kama Kombe la Azam Sports Federation Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam,
Ilimtangaza mshindi wa mwezi wa December, 2015 Ibrahim Ajib ambapo amepata kura nyingi zaidi zilizopigwa na mashabiki na wapenzi wa Simba na soka wa Tanzania kwa ujumla kupitia simu za mkononi ambao pia wamejiunga na huduma ya Simba News.